Sunday, October 25, 2009

FLEVA Djs Ndani ya FUJI DISCO TAKE WIKI HII





Wale watoaji wa ladha za pekee kali za muziki hapa visiwani Zanzibar (FLEVA DJ)
Wiki hii wataporomosha show la nguvu ambalo litakonga nyoyo za mashabiki wa burudani visiwani hapa
Katika kuupamba usiku huo utapata kujua kwanini Dorica amemchomolea jamaa kwa ngoma yake iliyong’ara ya “siwezi”

Rico single atawachana laivu wale wanao ongea ongea kupitia ngoma yake matata “acha waongee’

Unataka kujua ni lini june july atadondoka tena visiwani, Juma20 atakupa jibu live live akiwa jukwaani.

Kwa kiingilio cha kawaida tu Tsh.3000, jukwaa litatikisika kwa ajili yako
Sio pengine ni ndani ya ukumbi wa maraha wa FUJI DISCO TAKE
Saa 5:00 usiku FLEVA DJ Wataanza kurembea mizinga na kutupa mawe mpaka miale ya jua ianze kuchomoza machoni mwako

Usikose kufurahia maujanja ya kucheza na mashine na show la kihistoria.
Mikandamizo itarushwa na Dj wakali kama Dj side,Dj Bhaa s,Dj sam (mjanja suplier) pamoja na Dj Ally.

No comments: