Sunday, March 7, 2010

MAKOCHALI KAIBA BEAT YA BULLET?


Kuna utata mkubwa umejaa kuhusiana na beat aliyotembea nayo Quik Racka Bullet kua beat hiyo imeibiwa Kwa mujibu wa Producer wa S&S record alieko marekan mkali STIGO...amabe Ndie alietengeneza ngoma hiyo... . Haya tuliyajua baada ya kupata email kutok kwa Stigo ambayo ilikuwa ikisema hivi-----
Nilidhani maproducer wa Tanzania wameendelea sana lakini nahisi it was wrong.miaka miwili iliyopita nilitengeneza beat nikaiita Block Running, nikaiuza kwenye lebo moja inaitwa Koch Entertainment iliyoko New York kwa makubaliano ya kuwa lazima kuwa, mtu yeyote atakaeichukua lazima kuwe na jina langu kama mtengenezaji wa beat hiyo.lakkini siku mbili zilizopita nilishtuka sana baada ya rafiki yangu kutoka tanzania kunitumia nyimbo ikiwa na beat ile ile niliyoitengeneza miaka miwili iliyopita!!!! na siku sikia jina langu katika ngoma hiyo nilichiskia ni marcochali tu, nikawapigia Koch Entertainment kuwauliza nini kinaendelea? nao walishangaa kusikia habari hiyo, wakaniambia niwatumie nyimbo hiyo na nimewatumia.wakaniuliza kama nilishawahi kuituma beat Mj records ya Dar-es-salaam? nikasema mi sijawahi!!!

Lakini niliiweka beat kwenye itunes ili watu wainunue na kuitumia kwa ajili ya promotion tu na si kwa biashara, lakini MJ wametumia bila ruhusa kutoka Koch Entertainment na hawakufata makubaliano kwamba atakaetumia lazima kuwe na jina langu kama mtengenaji wa beat hiyo.sina haki yoyote ya kulalamika kwa MJ ila nitakacho fanya nikuwapeleka KOCH mahakamani na wao ndio watadili na Mj records.Ila nitadili na mj kama waliinunua kupitia itunes na kama ndio hivyo kwanini wameitumia ki biashara.

Haya wadau nadhna mnaham kubwa ya kutaka kujua ukweli upo wapi.. Ntajitahid kumtafuta makochali atwambie ilikuwaje?

No comments: