Sunday, December 27, 2009

TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA 2010 LAWIVA



Mtanange wa saba wa tamasha la Sauti za Busara ambalo hufanyika Zanzibar kila mwaka itakuwa ni kuanzia tarehe 11 hadi 16 Februari 2010; hakutakuwa na kiingilio kwa watakaoingia kabla saa kumi na moja.

Sauti za Busara ni tamasha la kimataifa ambalo linautambulisha na kuutangaza muziki wa Afrika Mashariki, na ambalo hufanyika katika kila wiki ya pili ya mwezi wa Februari kila mwaka kisiwani Zanzibar

Likionyesha wasanii maarufu na wanaochipukia na waliofanyiwa uteuzi makini zaidi ya 400 (vikundi 40 kwa jumla), Sauti za Busara imeweza kuthibitisha kuwa ni tukio kubwa na bora zaidi la muziki hapa Afrika mashariki, ni tukio linalowaunganisha watu katika mazingira ya kusherehekea.

HAWA NDIO WASANII HADI SASA WATAKAO KAMUA 2010
Thandiswa (South Africa) Malick Pathé Sow (Senegal) Fresh Jumbe & African Express (Tanzania / Japan) Simba & Brown Band (Mozambique) Banana Zorro & the B Band (Tanzania) Nyota Ndogo (Kenya) Jimmy Omonga (DRC / NL) Jhikoman (Tanzania) Mzungu Kichaa (Denmark / Tanzania) Makadem (Kenya) Ikwani Safaa Musical Club ft Tamalyn Dallal (Zanzibar / USA) Del & Diho (Mayotte) Mari Boine (Norway) Dawda Jobarteh (The Gambia) Sousou & Maher Cissoko (Senegal / Sweden) Xova (UK) Massar Egbari (Egypt) Debo Band (Ethiopia / USA) Bamba Nazar & The Pilgrimage (Suriname / NL) Joel Sebunjo & Sundiata (Uganda) Juliana Kanyomozi (Uganda) Maureen Lupo Lilanda (Zambia) Tausi Women's Taarab (Zanzibar) Mim Suleiman (Zanzibar / UK) Swifatui Abraar Group (Tanzania) DJ Eddy (Zanzibar) DJ Yusuf (UK / Zanzibar) Sowers Group (Tanzania) Best of WaPi (Tanzania) Sosolya Dance Academy (Uganda) Mapacha Africa (Kenya) Sinachuki Kidumbak (Zanzibar) Shirikisho Sanaa (Zanzibar) Tunaweza Band (Tanzania) KVZ Tupendane (Pemba) Keita & Swahili Vibes (Zanzibar) Maia Von Lekow (Kenya) na wengineo.

No comments: