Thursday, May 6, 2010

KISA CHA MPEMBA COMEDY !!

FLEVA DJS MORE THAN DJS
……bruuum bruum bruuuum….
…taxi ya Kengeja inakuja….
…mbele kuna polisi wa trafiki….
……mara polisi akaisimamisha gari…..
Polisi: “assalaam alaykum nzee”
Dereva: “wa alayku nsalaamu”
Polisi: “nakushtaki……kushajua kosalo?”
Dereva: “abaa hadi sasa sijajua…..na kwanjionavyo leo sinakosa”
Polisi: “unzidisha abiria abaa…wakubaliana namie?”
Dereva: “yakhe mie sijazidisha….nionyeshe huyo ntu aliezidi humu”
Polisi: “gariyo inruhusiwa kuchukua watu wanne….hebu esabu watuwo n’wangapi?”
Dereva: “n’wanane”
Polisi: “kutokana hesabuyo huoni kama watu wanne wanzidi hapo?”
Dereva: “nasema tena abaa sijazidisha…ila weye wajua kusoma?….subiri ntoke huko nje”
….dereva akatoka nje ya gari….
Dereva: “soma hapa nlangoni panaandikwaje?”
Polisi: “licensed to carry four passengers”
Dereva: “ha unjua maanaye?”
Polisi: “ehee…..inruhusiwa kuchukua abiria wane….ndio nkakwambia unzidisha abaa”
Dereve: “zunguka na nlango wa huku…uje usome…”
……dereva na polisi wakazunguka mlango wa mbele wa pili wa gari…”
Dereva: “haya soma hapa”
Polisi: “licensed to carry four passengers”
Dereva: “haya abaa nne na nne n’ngapi?”
Polisi: “n’nane
FLEVA DJS MORE THAN DJS

No comments: