Wednesday, January 20, 2010

SALON YA MASTAA ZANZIBAR


Kwa wale watanashati wanaweza kwenda katika salon ya LAAZIZI HAIR CUTTING SALON iliyopo mitaa ya kwa mchina mwanzo hapa hapa kutoka visiwa vyetu vya marashi ya karafuu.

Usijiulize masuali mengi sana mtu mzima hiyo ni salon inayokwenda na wakati kutokana na huduma zake nzuri na mukidee.

Ukiingia tu unajihisi kama uko Mbele kwa mbele vile, kumbe ni hapa hapa Unguja baba ake mimi mwenyewe nilioshuhudia kwa macho yuangu wakubwa wa nchi na heshima zao wakipata huduma pale, watangazaji wa radio stations tofauti, watoto wa vigogo na hata akina sisi pia tunakaribishwa kwa sababu bei zao ni nafuu.




Kama huamini angalia picha hizo ambazo zinakuonesha jinsi wakubwa walivyobobea katika kazi yao na walivyomakini katika kuuendeleza usemi uleeeee wa mteja ni mfalme.

Wanaotoa Huduma ni Mkali Ayub , Mkali Stopaaa. Mkali Rama.. Uspiiiiiiiiiimee!! Oi

No comments: